Habari

  • SERIKALI YAJA NA MKAKATI WA CHANJO ZA MAGONJWA MUHIMU YA MIFUGO KOTE NCHINI

    December 16, 2020

    Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul ameagiza kuandaliwa kwa mkakati shirikishi wa kupeleka chanjo kwa wafugaji kuanzia mwezi Februari Mwaka 2021 kupitia programu za chanjo ya magonjwa muhimu zitakazosimamiwa na wizara.

  • NARCO YAANZA KUTEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI, YACHANJA NG’OMBE ZAIDI YA 9000

    December 16, 2020

    Katika hatua za kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki Disemba 11, 2020, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) imeshaanza kutekeleza sehemu ya maagizo kwa kuwapatia chanjo ya homa ya mapafu (CBPP) ng’ombe wote 9, 237 waliopo katika Ranchi ya Kongwa iliyopo jijini Dodoma.

  • WAZIRI MASHIMBA ATOA MAAGIZO 3 KUDHIBITI HOMA YA MAPAFU KWA NG’OMBE

    December 16, 2020

    Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amemuagiza Kaimu Meneja Mkuu, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Maselle Shilagi kuhakikisha anawapa chanjo Ng’ombe wote katika Ranchi 14 za Taifa ili kuwakinga na ugonjwa wa homa ya mapafu ulioanza kuathiri baadhi ya Ng’ombe katika Ranchi ya Kongwa.

  • WATUMISHI WA WIZARA WAHIMIZWA USHIRIKIANO

    December 16, 2020

    Waziri Mteule wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amewataka Watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa ushirikiano kuhakikisha sekta hizo mbili zinachangia kwa sehemu kubwa katika maendeleo ya nchi na watu wake.

.