Nifanyeje?
- Zipi sifa za kuorodheshwa kama msaidizi wa mtaalam wa mifugo? (Enlisted Paraprofessional Assistant)
- Zipi sifa za kujiandikisha kama mtaalam msaidizi wa mifugo? (Enrolled Paraprofessional).
- Daktari wa mifugo asiye mtanzania (Foreigner) anasajiliwa vipi na Baraza.
- Daktari wa mifugo asiye Mtanzania anaweza kusajiliwa na kufanyakazi hapa nchini? (Temporary and permanent registration)?
Albamu ya Video
-
Wadau wakieleza faida ya mafunzo ya ufugaji bora
June 17, 2020Wadau wakieleza faida ya mafunzo ya ufugaji bora
-
"Tumejadiliana uwekezaji katika sekta ya uvuvi." Bw. Bulayi
June 10, 2020Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bw. Emmanuel Bulayi amefanya mazungumzo na ugeni kutoka Benki ya Maendeleo ya (AfDB) ukiongozwa na Mkurugenzi wa Masuala ya sekta za kilimo na Maendeleo Vijijini Bi. Toda Atsuko, Mkurugenzi Mkaazi wa benki hiyo hapa nchini Dkt. Alex Mubiru pamoja na maafisa wengine kutoka katika benki hiyo. Kikao hicho kilichofanyika katika ofisi za wizara hiyo Mtumba jijini Dodoma (06.02.2020) kimehudhuriwa pia na maafisa kutoka Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi
-
"Wizara inataka uwekezaji utakaoinua uchumi wa wafugaji." Katibu Mkuu Prof. Gabriel
June 10, 2020Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amefanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Masuala ya Sekta za Kilimo na Maendeleo Vijijini kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Bi. Toda Atsuko pamoja na maafisa wengine kutoka katika benki hiyo, Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, akisisitiza uwekezaji wa benki hiyo katika sekta ya mifugo ili kuinua uchumi wa wafugaji. Mazungumzo hayo yamefanyika katika ofisi za wizara hiyo zilizopo mji wa serikali Mtumba jijini Dodoma. (05.02.2020)
-
KIPINDI: MIFUGO NA UVUVI (NAMNA MALIGHAFI ZA MIFUGO ZINAVYOONGEZEWA THAMANI)
June 10, 2020Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaandaa mfululizo wa vipindi vya redio na televisheni ambavyo lengo lake kuu ni kutoa elimu na kukufahamisha majukumu ya wizara ya kuboresha sekta ya mifugo na uvuvi kwa mwananchi na taifa kwa ujumla. Katika kipindi hiki utafahamu namna malighafi za mifugo zinavyoongezewa thamani kupitia viwanda vilivyopo hapa nchini kikiwemo kiwanda cha 'Happy Sausage' ambacho kinachomilikiwa na mtanzania.
-
"Kafanyeni kazi kwa ufanisi na muhakikishe mnakusanya mapato." Prof. Gabriel
June 10, 2020Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel 05.02.2020 amefungua kikao cha kupitia taarifa ya utekelezaji wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2019/2020 na mpango na bajeti kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kwa maafisa kutoka vituo vya mifugo (ZVC), minada ya upili na mipakani na maeneo ya mikakati. Kikao hicho kimefanyika kwa siku mbili katika ofisi za wizara hiyo zilizopo katika mji wa serikali Mtumba jijini Dodoma.